يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَخُونُواْ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَ وَتَخُونُوٓاْ أَمَٰنَٰتِكُمۡ وَأَنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
Enyi mlio amini! Msimfanyie khiana Mwenyezi Mungu na Mtume, wala msikhini amana zenu, nanyi mnajua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na makazifuata sheria Zake kivitendo, msimhini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake kwa kuyaacha Aliyowalazimisha nayo na kuyafanya Aliyowakataza nayo, na wala msifanye kasoro katika yale ambayo Mwenyezi Mungu Aliwaamini nayo, na hali nyinyi mnajua kwamba ni amana inayopasa kutekelezwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس