يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا لَقِيتُمۡ فِئَةٗ فَٱثۡبُتُواْ وَٱذۡكُرُواْ ٱللَّهَ كَثِيرٗا لَّعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ
Enyi mlio amini! Mkikutana na jeshi, basi kueni imara, na mkumbukeni Mwenyezi Mungu sana ili mpate kufanikiwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi mliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na mkazifuata sheria Zake kivitendo, mkutanapo na kundi la watu wa ukafiri wakawa wamejitayarisha kupigana na nyinyi, basi thibitini na msishindwe na wao na mumtaje Mwenyezi Mungu kwa wingi, hali ya kuomba na kunyenyekea, Awateremshie ushindi na uwezo wa kumshinda adui yenu, ili mufaulu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس