وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بَعۡضُهُمۡ أَوۡلِيَآءُ بَعۡضٍۚ إِلَّا تَفۡعَلُوهُ تَكُن فِتۡنَةٞ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَفَسَادٞ كَبِيرٞ
Na wale walio kufuru ni marafiki wenyewe kwa wenyewe. Msipo fanya hivi itakuwako fitna katika nchi na fisadi kubwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wale waliokanusha, ni wenye kusaidiana wao kwa wao. Na iwapo hamtakuwa, enyi Waumini, ni wenye kusaidiana nyinyi kwa nyinyi, basi kutapatikana katika ardhi kufitiniwa Waumini na dini ya Mwenyezi Mungu na uharibifu mkubwa wa kuzuiwa njia ya Mwenyezi Mungu na kutiwa nguvu misingi ya ukafiri.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس