وَإِن كُنتُنَّ تُرِدۡنَ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ وَٱلدَّارَ ٱلۡأٓخِرَةَ فَإِنَّ ٱللَّهَ أَعَدَّ لِلۡمُحۡسِنَٰتِ مِنكُنَّ أَجۡرًا عَظِيمٗا
Na ikiwa mnamtaka Mwenyezi Mungu na Mtume wake na nyumba ya Akhera, basi Mwenyezi Mungu amewaandalia wafanyao mema, miongoni mwenu, malipo makubwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Na mkiwa mnataka radhi ya Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na yale aliyowaandalia Mwenyezi Mungu katika Nyumba ya Akhera, basi vumilieni juu ya hali mliyonayo, na mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, kwani hakika Mwenyezi Mungu Amewaandalia walio wema katika nyinyi malipo makubwa.» (Na walimchagua Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na yale Aliyowaandalia Mwenyezi Mungu katika Nyumba ya Akhera).
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس