وَسَبِّحُوهُ بُكۡرَةٗ وَأَصِيلًا
Na mtakaseni asubuhi na jioni.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na zishughulisheni nyakati zenu kwa kumtaja Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, asubuhi na jioni, baada ya Swala za faradhi na nyakati za matukio maalumu na sababu, kwani huko kumtaja Mwenyezi Mungu ni ibada iliowekwa na Sheria, inapelekea kwenye mapenzi ya Mwenyezi Mungu na kujizuia na madhambi, na inasaidia kila kheri.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس