ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِٱلۡكِتَٰبِ وَبِمَآ أَرۡسَلۡنَا بِهِۦ رُسُلَنَاۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ
Ambao wamekanusha Kitabu na yale tuliyo watuma Mitume wetu. Basi watakuja jua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Washirikina hawa waliokanusha Qur’ani na Vitabu vya mbinguni Alivyoviteremsha Mwenyezi Mungu kwa Mitume Wake ili kuongoza watu, watajua wakanushaji hawa mwisho wa ukanushaji wao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس