وَٱلَّذِينَ يُحَآجُّونَ فِي ٱللَّهِ مِنۢ بَعۡدِ مَا ٱسۡتُجِيبَ لَهُۥ حُجَّتُهُمۡ دَاحِضَةٌ عِندَ رَبِّهِمۡ وَعَلَيۡهِمۡ غَضَبٞ وَلَهُمۡ عَذَابٞ شَدِيدٌ
Na wanao hojiana juu ya Mwenyezi Mungu baada ya kukubaliwa, hoja za hawa ni baat'ili mbele ya Mola wao Mlezi, na juu yao ipo ghadhabu, na itakuwa kwao adhabu kali.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wale wanaojadili kuhusu Dini ya Mwenyezi Mungu niliyomtumiliza kwayo Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, baada ya watu kuikubali na kusilimu, hoja yao na mjadala wao, mbele ya Mola wao, ni zenye kutenguka na kuondoka. Na watashukiwa na adhabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu hapa duniani, na huko Akhera watakuwa na adhabu kali, nayo ni Moto.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس