وَإِذۡ صَرَفۡنَآ إِلَيۡكَ نَفَرٗا مِّنَ ٱلۡجِنِّ يَسۡتَمِعُونَ ٱلۡقُرۡءَانَ فَلَمَّا حَضَرُوهُ قَالُوٓاْ أَنصِتُواْۖ فَلَمَّا قُضِيَ وَلَّوۡاْ إِلَىٰ قَوۡمِهِم مُّنذِرِينَ
Na wakati tulipo waleta kundi la majini kuja kwako kusikiliza Qur'ani. Basi walipo ihudhuria walisema: Sikilizeni! Na ilipo kwisha somwa, walirudi kwa kaumu yao kwenda kuwaonya.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kumbuka, ewe Mtume, pindi tulipokutumia kundi la majini kusikiliza Qur’ani kutoka kwako. Walipohudhuria, na Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, yuwasoma, waliambiana wao kwa wao, «Nyamazeni tusikilize Qur’ani! Na Mtume Alipomaliza kusoma Qur’ani, na wao wakawa wameielewa na ikawa imewaathiri, walirudi kwa majini wenzao wakawaonya na kuwahadharisha adhabu ya Mwenyezi Mungu wasipoamini.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس