وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ وَءَامَنُواْ بِمَا نُزِّلَ عَلَىٰ مُحَمَّدٖ وَهُوَ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّهِمۡ كَفَّرَ عَنۡهُمۡ سَيِّـَٔاتِهِمۡ وَأَصۡلَحَ بَالَهُمۡ
Na walio amini, na wakatenda mema, na wakaamini aliyo teremshiwa Muhammad - nayo ni Haki iliyo toka kwa Mola wao Mlezi - atawafutia makosa yao na ataitengeneza hali yao.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na wakafuata Sheria Zake na wakaamini Kitabu Alichomteremshia Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, nacho ndio ukweli usiokuwa na shaka kutoka kwa Mola wao, Mwenyezi Mungu Atawasamehe na Atawafinikia maovu waliyoyafanya na hatawatesa kwa maovu hayo na Atawatengezea mambo yao duniani na Akhera.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس