إِنَّ ٱلَّذِينَ ٱرۡتَدُّواْ عَلَىٰٓ أَدۡبَٰرِهِم مِّنۢ بَعۡدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُمُ ٱلۡهُدَى ٱلشَّيۡطَٰنُ سَوَّلَ لَهُمۡ وَأَمۡلَىٰ لَهُمۡ
Kwa hakika wanao rudi nyuma baada ya kwisha wabainikia uwongofu, Shetani huyo amewashawishi na amewaghuri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika ya wale waliyorudi nyuma wakaacha uongofu na Imani na wakageuka kwa visigino vyao wakimkanusha Mwenyezi Mungu baada ya haki kuwafunukia, (hao) Shetani amewapambia makosa yao na akawanyoshea matumaini ya kuishi duniani.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس