لِّئَلَّا يَعۡلَمَ أَهۡلُ ٱلۡكِتَٰبِ أَلَّا يَقۡدِرُونَ عَلَىٰ شَيۡءٖ مِّن فَضۡلِ ٱللَّهِ وَأَنَّ ٱلۡفَضۡلَ بِيَدِ ٱللَّهِ يُؤۡتِيهِ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ ذُو ٱلۡفَضۡلِ ٱلۡعَظِيمِ
Ili watu wa Kitabu wajue kwamba wao hawana uweza wowote juu ya fadhila za Mwenyezi Mungu. Na fadhila zote zimo mikononi mwa Mwenyezi Mungu. Humpa amtakaye. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye fadhila kuu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Amewapa haya yote ili wapate kujua watu waliopewa Vitabu ambao hawakumuamini Mtume Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, kwamba wao hawawezi chochote kujipa wao wenyewe nyongeza za kheri za Mwenyezi Mungu wala kuwapatia wengine, na kwamba nyongeza zote ziko kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye wema mkubwa na vipewa vingi kwa viumbe Vyake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس