وَمَا جَعَلَهُ ٱللَّهُ إِلَّا بُشۡرَىٰ وَلِتَطۡمَئِنَّ بِهِۦ قُلُوبُكُمۡۚ وَمَا ٱلنَّصۡرُ إِلَّا مِنۡ عِندِ ٱللَّهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ
Na Mwenyezi Mungu hakufanya haya ila kuwa ni bishara na ili nyoyo zenu zituwe. Na haupatikani ushindi ila kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, na Mwenye hikima.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu Hakuufanya msaada huo usipokuwa ni bishara kwenu ya ushindi na ili nyoyo zenu zitulie na muwe na yakini ya kupata ushindi kutoka kwa Mwenyezi Mungu, kwani ushindi watoka kwa Mwenyezi Mungu tu, si kwa ukali wa zana zenu na nguvu zenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mshindi katika ufalme Wake ni Mwenye hekima katika upelekeshaji Wake na uwekaji sheria Wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس