وَإِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتُنَا قَالُواْ قَدۡ سَمِعۡنَا لَوۡ نَشَآءُ لَقُلۡنَا مِثۡلَ هَٰذَآ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّآ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ
Na wanapo somewa Aya zetu, wao husema: Tumesikia. Na lau tungeli penda tunge sema kama haya. Haya si chochote ila hadithi za watu wa kale tu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na pindi wanaposomewa, hawa ambao walimkanusha Mwenyezi Mungu, aya za Qur’ani tukufu, wao husema kwa ujinga wao na kuikejeli kwao haki, «Tumeshalisikia hili hapo nyuma, na lau tunataka tungalisema maneno yafananayo na hii Qur’ani. Haikuwa Qur’ani hii unayotusomea, ewe Muhammad, isipokuwa ni maneno ya urongo ya watu wa kale.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس