وَإِذۡ يُرِيكُمُوهُمۡ إِذِ ٱلۡتَقَيۡتُمۡ فِيٓ أَعۡيُنِكُمۡ قَلِيلٗا وَيُقَلِّلُكُمۡ فِيٓ أَعۡيُنِهِمۡ لِيَقۡضِيَ ٱللَّهُ أَمۡرٗا كَانَ مَفۡعُولٗاۗ وَإِلَى ٱللَّهِ تُرۡجَعُ ٱلۡأُمُورُ
Na mlipo kutana akakuonyesheni machoni mwenu kuwa wao ni wachache, na akakufanyeni nyinyi ni wachache machoni mwao, ili Mwenyezi Mungu atimize jambo lilio kuwa liwe. Na mambo yote hurejezwa kwa Mwenyezi Mungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kumbuka pia pindi walipojitokeza maadui kwenye ardhi ya mapigano mkawaona kuwa ni wachache mkawa na ujasiri juu yao, na Akawafanya nyinyi ni wachache kwenye macho yao, ili waache kujiandaa kupigana na nyinyi, ili Mwenyezi Mungu Alipitishe jambo ambalo hapana budi lifanyike, ili itimie ahadi ya Mwenyezi Mungu kwenu ya himaya na ushindi. Hapo likawa neno la Mwenyezi Mungu ndilo la juu, na neno la wale waliokanusha ndilo la chini, Na kwa Mwenyezi Mungu ndiko marudio ya mambo yote, Apate kumlipa kila mmoja kwa anachostahili kulipwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس