كَدَأۡبِ ءَالِ فِرۡعَوۡنَ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۚ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ فَأَخَذَهُمُ ٱللَّهُ بِذُنُوبِهِمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ قَوِيّٞ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ
Kama ada ya watu wa Firauni na walio kuwa kabla yao - walizikataa Ishara za Mwenyezi Mungu. Basi Mwenyezi Mungu aliwashika kwa sababu ya madhambi yao. Na hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na mkali wa kuadhibu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika yale yaliyowapata washirikina siku hiyo ndio mwendo wa Mwenyezi Mungu katika kuwatia adabu wakiukaji mipaka miongoni mwa umma waliotangulia, mfano wa Fir'awn na waliomtangulia, walipowakanusha Mitume wa Mwenyezi Mungu na wakazipinga aya Zake. Kwa hakika Mwenyezi Mungu Aliwateremshia mateso Yake kwa sababu ya madhambi yao. Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Asiyeshindwa, ni Mkali wa mateso kwa aliyemuasi na asitubie kutokana na dhambi zake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس