كَدَأۡبِ ءَالِ فِرۡعَوۡنَ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡۚ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِ رَبِّهِمۡ فَأَهۡلَكۡنَٰهُم بِذُنُوبِهِمۡ وَأَغۡرَقۡنَآ ءَالَ فِرۡعَوۡنَۚ وَكُلّٞ كَانُواْ ظَٰلِمِينَ
Ni kama ada ya watu wa Firauni na walio kabla yao - walizikanusha Ishara za Mola wao Mlezi, basi tukawateketeza kwa madhambi yao. Na tukawazamisha watu wa Firauni. Na wote walikuwa wenye kudhulumu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hali ya Makafiri hawa ni kama hali ya Makafiri wa jamaa za Fir'awn ambao walimkanusha Mūsā, na ni kama hali ya wale waliowakanusha Mitume wao miongoni mwa watu waliopita. Mwenyezi Mungu Aliwaangamiza kwa sababu ya madhambi yao na Akawazamisha jamaa za Fir'awn baharini. Na kila umma kati yao walikuwa wanatenda mambo ambayo haikufaa wao kuyatenda, ya kukanusha kwao Mitume wa Mwenyezi Mungu na kupinga kwao aya za Mwenyezi Mungu na kushirikisha kwao, katika ibada, asiyekuwa Yeye.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس