وَلَقَدۡ كَانُواْ عَٰهَدُواْ ٱللَّهَ مِن قَبۡلُ لَا يُوَلُّونَ ٱلۡأَدۡبَٰرَۚ وَكَانَ عَهۡدُ ٱللَّهِ مَسۡـُٔولٗا
Na hakika walikwisha muahidi Mwenyezi Mungu kabla yake kwamba hawatageuza migongo yao. Na ahadi ya Mwenyezi Mungu ni yenye kuulizwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kwa hakika, wanafiki hawa walimuahidi Mwenyezi Mungu kupitia kwa Mtume Wake kabla ya vita vya Shimo (Khandaq) kuwa hawatakimbia watakapohudhuria vita na hawatachelewa watakapoitwa kwenda Jihadi, lakini wao walihini ahadi yao. Na Mwenyezi Mungu Atawahesabu kwa hilo na Atawauliza kuhusu ahadi hiyo. Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu itaulizwa na itahesabiwa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس