وَأَنزَلَ ٱلَّذِينَ ظَٰهَرُوهُم مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ مِن صَيَاصِيهِمۡ وَقَذَفَ فِي قُلُوبِهِمُ ٱلرُّعۡبَ فَرِيقٗا تَقۡتُلُونَ وَتَأۡسِرُونَ فَرِيقٗا
Na akawateremsha wale walio wasaidia (maadui) katika Watu wa Kitabu kutoka katika ngome zao; na akatia khofu katika nyoyo zao. Baadhi yao mkawa mnawauwa, na wengine mnawateka.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Mwenyezi Mungu Akawateremsha Mayahudi wa Banū Qurayẓah kutoka kwenye ngome zao kwa kuwa waliyasaidia Mapote katika kupigana na Waislamu, na Akatia hofu ndani ya nyoyo zao wakashindwa, mkawa mnaua kundi katika wao na mnateka kundi lingine.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس