يَٰنِسَآءَ ٱلنَّبِيِّ مَن يَأۡتِ مِنكُنَّ بِفَٰحِشَةٖ مُّبَيِّنَةٖ يُضَٰعَفۡ لَهَا ٱلۡعَذَابُ ضِعۡفَيۡنِۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عَلَى ٱللَّهِ يَسِيرٗا
Enyi wake wa Nabii! Atakaye fanya uchafu dhaahiri miongoni mwenu, atazidishiwa adhabu mara mbili. Na hayo kwa Mwenyezi Mungu ni mepesi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Enyi wake za Mtume! Yoyote miongoni mwenu Atakayefanya maasia yaliyo wazi ataongezewa adhabu mara mbili zaidi.( Na kwa kuwa cheo chao ni cha juu, imenasibiana na cheo hicho Mwenyezi Mungu Alifanye dhambi linalotokana na wao liwe zito, ili kuhifadhi heshima yao na heshima ya Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, Na kuadhibu huko ni rahisi kwa Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس