وَٱذۡكُرۡنَ مَا يُتۡلَىٰ فِي بُيُوتِكُنَّ مِنۡ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ وَٱلۡحِكۡمَةِۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ لَطِيفًا خَبِيرًا
Na kumbukeni yasomwayo majumbani mwenu katika Aya za Mwenyezi Mungu na hikima. Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa mambo ya siri, na Mwenye khabari.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na yatajeni yale yanayosomwa ndani ya majumba yenu, ya Qur’ani na hadithi za Mtume, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukiena muyafanyie kazi na muyape cheo ambacho yanastahiki., kwani hayo ni miongoni mwa neema za Mwenyezi Mungu kwenu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mpole kwenu, kwa kuwa Amewaweka majumbani ambako aya za Mwenyezi Mungu zinasomwa na Sunnah, ni Mtambuzi wa kuwatambua nyinyi kwa kuwachagua muwe wake wa Mtume Wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس