مَّا كَانَ عَلَى ٱلنَّبِيِّ مِنۡ حَرَجٖ فِيمَا فَرَضَ ٱللَّهُ لَهُۥۖ سُنَّةَ ٱللَّهِ فِي ٱلَّذِينَ خَلَوۡاْ مِن قَبۡلُۚ وَكَانَ أَمۡرُ ٱللَّهِ قَدَرٗا مَّقۡدُورًا
Hapana ubaya kwa Nabii kufanya aliyo mhalalishia Mwenyezi Mungu. Huo ndio mwendo wa Mwenyezi Mungu kwa walio pita zamani. Na amri ya Mwenyezi Mungu ni kudura iliyo kwisha kadiriwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Haikuwa ni dhambi kwa Nabii Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, katika kile Alichomhalalishia Mwenyezi Mungu cha kumuoa mke wa mwanawe wa kujibandika baada ya kumuacha, kama vile alivyowahalalishia hilo Manabii kabla yake yeye, ni mwenendo uliowekwa na Mwenyezi Mungu kwa wale waliopita kabla. Na kwa kweli, amri ya Mwenyezi Mungu ni mpango uliokadiriwa , hauna budi kutokea.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس