ٱلَّذِينَ يُبَلِّغُونَ رِسَٰلَٰتِ ٱللَّهِ وَيَخۡشَوۡنَهُۥ وَلَا يَخۡشَوۡنَ أَحَدًا إِلَّا ٱللَّهَۗ وَكَفَىٰ بِٱللَّهِ حَسِيبٗا
(Hao wa zamani) walio kuwa wakifikisha risala za Mwenyezi Mungu na wanamwogopa Yeye, na wala hawamwogopi yeyote isipo kuwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ndiye atoshaye kuhisabu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kisha Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika, Aliwataja Manabii waliopita na Akawasifu kwamba wao ni wale wanaozifikisha jumbe za Mwenyezi Mungu kwa watu, na wanamuogopa Mwenyezi Mungu, Peke Yake, na hawamuogopi yoyote asiyekuwa Yeye. Na inatosha kuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye kuwahesabu waja Wake kwa matendo yao yote na ni Mwenye kuyaona.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس