لَّا جُنَاحَ عَلَيۡهِنَّ فِيٓ ءَابَآئِهِنَّ وَلَآ أَبۡنَآئِهِنَّ وَلَآ إِخۡوَٰنِهِنَّ وَلَآ أَبۡنَآءِ إِخۡوَٰنِهِنَّ وَلَآ أَبۡنَآءِ أَخَوَٰتِهِنَّ وَلَا نِسَآئِهِنَّ وَلَا مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُنَّۗ وَٱتَّقِينَ ٱللَّهَۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدًا
Hapana ubaya kwao (wake za Mtume) kuonana na baba zao, wala watoto wao, wala ndugu zao, wala watoto wa ndugu zao wanaume, wala watoto wa ndugu zao wanawake, wala wanawake wenzao, wala wale iliyo wamiliki mikono yao ya kulia. Na enyi wanawake, mcheni Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kushuhudia kila kitu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakuna dhambi kwa wanawake kutojifinika mbele ya baba zao, wana wao wa kiume,ndugu zao wa kiume, wana wa kiume wa ndugu zao wa kiume, wana wa kiume wa ndugu zao wa kike, wanawake waumini na watumwa waliomilikiwa na wao kwa kuwa wanahitaji utumishi wao sana. Na muogopeni Mwenyezi Mungu , enyi wanawake, msipite mpaka mliowekewa mkaonyesha pambo lenu msiofaa kulionyesha, au mkaacha kujifinika mbele ya yule ambaye ni lazima mjifinike mbele yake. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kushuhudia kila kitu, Anashuhudia matendo ya waja , ya nje na ya ndani, na Atawalipa kwayo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس