۞فَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّن كَذَبَ عَلَى ٱللَّهِ وَكَذَّبَ بِٱلصِّدۡقِ إِذۡ جَآءَهُۥٓۚ أَلَيۡسَ فِي جَهَنَّمَ مَثۡوٗى لِّلۡكَٰفِرِينَ
BASI NI NANI dhaalimu mkubwa kuliko yule aliye msingizia uwongo Mwenyezi Mungu na kuikanusha kweli imfikiapo? Je! Siyo katika Jahannamu makaazi ya hao makafiri?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakuna yoyote dhalimu zaidi kuliko yule aliyemzulia Mwenyezi Mungu urongo, kwa kumnasibishia sifa isiyofaa kusifika nayo, kama vile kuwa na mshirika na mtoto, au akasema, «Mimi nimeletewa wahyi,» na hali yeye hakuletewa wahyi wa kitu chochote. Na hakuna dhalimu zaidi kuliko yule aliyeikanusha haki iliyoteremka kwa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie. Kwani si yako huko Motoni mashukio na makazi kwa waliomkufuru Mwenyezi Mungu na wasimuamini Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie? Ndio, yako.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس