وَبَدَا لَهُمۡ سَيِّـَٔاتُ مَا كَسَبُواْ وَحَاقَ بِهِم مَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ
Na utawadhihirikia ubaya wa waliyo yachuma, yatawazunguka waliyo kuwa wakiyafanyia mzaha.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na yatawadhihirikia hao wakanushaji, Siku ya kuhesabiwa, malipo ya maovu yao waliyoyatenda, kwa kuwa walimnasibishia Mwenyezi Mungu sifa isiyolingana na Yeye, na wakafanya maasia katika maisha yao, na itawazunguka adhabu kali kila upande ikiwa ni mateso kwao kwa kulifanyia shere onyo la adhabu ambayo Mtume alikuwa akiwaahidi kuwa itawapata wakawa hawaitii maanani.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس