وَيُنَجِّي ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ بِمَفَازَتِهِمۡ لَا يَمَسُّهُمُ ٱلسُّوٓءُ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ
Na Mwenyezi Mungu atawaokoa wenye kujikinga kwa ajili ya kufuzu kwao. Hapana uovu utao wagusa, wala hawatahuzunika.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Mwenyezi Mungu Atawaokoa na Moto wa Jahanamu na adhabu yake wale waliomcha Mola wao kwa kutekeleza faradhi Alizoziamrisha na kujiepusha na yale Aliyoyakataza kwa kufuzu kwao na kutimia matakwa yao, nako ni kufaulu kupata Pepo. Hawataguswa na kitu chochote cha adhabu wala hawatazisikitikia hadhi za duniani walizozikosa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس