ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ كَرِهُواْ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ فَأَحۡبَطَ أَعۡمَٰلَهُمۡ
Hayo ni kwa sababu waliyachukia aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu, basi akaviangusha vitendo vyao.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hayo ni kwa sababu wao walikichukia Kitabu cha Mwenyezi Mungu kilichoteremshwa kwa Mtume Wake Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, wakakikanusha, na Mwenyezi Mungu akayatangua matendo yao kwa kuwa yalikuwa katika kumtii Shetani.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس