مَا جَعَلَ ٱللَّهُ مِنۢ بَحِيرَةٖ وَلَا سَآئِبَةٖ وَلَا وَصِيلَةٖ وَلَا حَامٖ وَلَٰكِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يَفۡتَرُونَ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَۖ وَأَكۡثَرُهُمۡ لَا يَعۡقِلُونَ
Mwenyezi Mungu hakujaalia uharamu wowote juu ya "Bahira" wala "Saiba" wala "Wasila" wala "Hami". Lakini walio kufuru humzulia uwongo Mwenyezi Mungu, na wengi wao hawatumii akili.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu Hakuwawekea washirikina yale waliyoyazua ya kuacha kunufaika na baadhi ya wanyama wa mifugo na kuwafanya ni wa masanamu. Nao ni baḥīrah: anayekatwa sikio lake akiwa amezaa idadi fulani ya watoto, sāibah: anayeachiwa masanamu, waṣīlah: ambaye amezaa watoto wa kike mfululizo na hāmī: ngamia dume iwapo, kutokana na yeye, wamazaliwa idadi fulani ya ngamia. Lakini makafiri waliyanasibisha hayo kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kwa kumzulia urongo. Na wengi wa makafiri hawapambanui baina ya haki na batili.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس