لِلَّهِ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا فِيهِنَّۚ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرُۢ
Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi na vilivyomo. Naye ni Muweza wa kila kitu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ni wa Mwenyezi Mungu Peke Yake ufalme wa mbinguni na ardhini na vilivyomo ndani yake, na Yeye, Aliyetakata na kila sifa mbaya, kwa kila kitu ni muweza; hakuna kitu kinachomshinda.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس