وَكَتَبۡنَا عَلَيۡهِمۡ فِيهَآ أَنَّ ٱلنَّفۡسَ بِٱلنَّفۡسِ وَٱلۡعَيۡنَ بِٱلۡعَيۡنِ وَٱلۡأَنفَ بِٱلۡأَنفِ وَٱلۡأُذُنَ بِٱلۡأُذُنِ وَٱلسِّنَّ بِٱلسِّنِّ وَٱلۡجُرُوحَ قِصَاصٞۚ فَمَن تَصَدَّقَ بِهِۦ فَهُوَ كَفَّارَةٞ لَّهُۥۚ وَمَن لَّمۡ يَحۡكُم بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ
Na humo tuliwaandikia ya kwamba roho kwa roho, na jicho kwa jicho, na pua kwa pua, na sikio kwa sikio, na jino kwa jino, na kwa majaraha kisasi. Lakini atakaye samehe basi itakuwa ni kafara kwake. Na wasio hukumu kwa yale aliyo yateremsha Mwenyezi Mungu, basi hao ndio madhaalimu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na tulilifanya ni lazima kwao katika Taurati kwamba mtu huuawa akiua mtu, hutolewa jicho akitoa jicho la mtu, hukatwa pua akikata pua ya mtu, hukatwa sikio akikata sikio la mtu, na hung’olewa jino aking’oa jino la mtu na kwamba hulipizwa kisasi kwa kutia mtu majaraha. Mwenye kusamehe haki yake ya kulipiza kisasi kwa aliyemfanyia uadui, basi huko ni kujifutia na kujiondolea sehemu ya madhambi ya yule aliyefanyiwa uadui. Na yule asiyehukumu kwa yaliyoteremshwa na Mwenyezi Mungu, katika kisasi na megineyo, basi hao ni wakiukaji wa mipaka ya Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس