لَيۡسَ عَلَى ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ جُنَاحٞ فِيمَا طَعِمُوٓاْ إِذَا مَا ٱتَّقَواْ وَّءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ ثُمَّ ٱتَّقَواْ وَّءَامَنُواْ ثُمَّ ٱتَّقَواْ وَّأَحۡسَنُواْۚ وَٱللَّهُ يُحِبُّ ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Si dhambi juu ya walio amini na wakatenda mema kwa walivyo vila (zamani) maadamu wakichamngu na wakiamini na wakitenda mema, kisha wakachamngu, na wakaamini, kisha wakachamngu na wakafanya mazuri. Na Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao mazuri.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Waumini waliokunywa pombe kabla haijaharamishwa hawana dhambi kwa kufanya hilo, iwapo wataiacha, wakajikinga na mambo yanayomkasirisha Mwenyezi Mungu na wakatanguliza matendo mema yanayoonyesha kuwa wao wanamuamini Yeye na wana hamu Mwenyezi Mungu, aliyetukuka, Awe radhi nao, kisha wakazidi kumtunza Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka, na kumuamini mpaka wakawa, kwa ile yakini yao, wanamuabudu kama kwamba wao wanamuona. Hakika Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anawapenda wale ambao wamefikia kiwango cha ihsani (iḥsān) mpaka wakawa kuiamini kwao ghaibu (al-ghayb) ni kama vile wanavyoyaamini wanayoyaona.[3]
____________________
[3]Rudia 2:3 kwa ufafanuzi wa al-ghyb.
____________________
[3]Rudia 2:3 kwa ufafanuzi wa al-ghyb.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس