مَّا عَلَى ٱلرَّسُولِ إِلَّا ٱلۡبَلَٰغُۗ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ مَا تُبۡدُونَ وَمَا تَكۡتُمُونَ
Haimlazimu Mtume ila kufikisha ujumbe tu. Na Mwenyezi Mungu anajua mnacho kidhihirisha na mnacho kificha.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, Anawaelezea kwamba shughuli ya Mtume Wake , rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, ni kuongoza kwa kuelekeza na kufikisha na kwamba uongofu wa taufiki uko mkononi mwa Mwenyezi Mungu, Peke Yake, na kwamba mambo yaliyomo ndani ya nafsi za watu, katika yale wanayoyafanya kwa siri na wanayoyatangaza, ya uongofu na upotevu, Mwenyezi Mungu Anayajua..
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس