وَإِذۡ يَمۡكُرُ بِكَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيُثۡبِتُوكَ أَوۡ يَقۡتُلُوكَ أَوۡ يُخۡرِجُوكَۚ وَيَمۡكُرُونَ وَيَمۡكُرُ ٱللَّهُۖ وَٱللَّهُ خَيۡرُ ٱلۡمَٰكِرِينَ
Na walipo kupangia mpango walio kufuru wakufunge, au wakuuwe, au wakutoe. Wakapanga mipango yao, na Mwenyezi Mungu akapanga yake. Na Mwenyezi Mungu ndiye mbora wa mipango.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kumbuka, ewe Mtume, wanapofanya njama washirikina wa Maka wakufunge au wakuue au wakuhamishe kutoka mjini kwako. Wanakufanyia njama, na Mwenyezi Mungu Aliwarudushia njama zao, ikiwa ni malipo yao, na Mwenyezi Mungu Anafanya njama; na Mwenyezi Mungu ni bora wa wenye kufanya njama.[5]
____________________
[5]Kwa kuwa njama za washirikina zinajulikana na Mwenyezi Mungu na kwa hivyo hazina athari yoyote, ndio maana ya kuwa Mwenyezi Mungu anafanya njama na kuwa njama zake zinashinda zao.
____________________
[5]Kwa kuwa njama za washirikina zinajulikana na Mwenyezi Mungu na kwa hivyo hazina athari yoyote, ndio maana ya kuwa Mwenyezi Mungu anafanya njama na kuwa njama zake zinashinda zao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس