وَمَا كَانَ ٱللَّهُ لِيُعَذِّبَهُمۡ وَأَنتَ فِيهِمۡۚ وَمَا كَانَ ٱللَّهُ مُعَذِّبَهُمۡ وَهُمۡ يَسۡتَغۡفِرُونَ
Na Mwenyezi Mungu hakuwa wa kuwaadhibu nawe umo pamoja nao, wala Mwenyezi Mungu si wa kuwaadhibu na hali ya kuwa wanaomba msamaha.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hakuwa Mwenyezi Mungu, Aliyetakata na sifa za upungufu na kutukuka, ni Mwenye kuwaadhibu washirikina hawa na hali wewe, ewe Mtume, uko pamoja nao, na hakuwa Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaadhibu wao na hali wao wanaomba msamaha wa madhambi yao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس