وَمَا كَانَ صَلَاتُهُمۡ عِندَ ٱلۡبَيۡتِ إِلَّا مُكَآءٗ وَتَصۡدِيَةٗۚ فَذُوقُواْ ٱلۡعَذَابَ بِمَا كُنتُمۡ تَكۡفُرُونَ
Na haikuwa ibada yao kwenye hiyo Nyumba (Al Kaaba) ila ni kupiga miunzi na makofi. Basi onjeni adhabu kwa vile mlivyo kuwa mkikufuru.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakukuwa kuswali kwao kwenye Msikiti wa H(arām isipokuwa ni kupiga mbinja na kupiga makofi, basi onjeni adhabu ya kuuawa na kutekwa siku ya Badr kwa sababu ya kukanusha kwenu na vitendo vyenu ambavyo hakuna mwenye kujitokeza kuvitenda isipokuwa makafiri wenye kukataa upweke wa Mola wao na utume wa Nabii wao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس