وَلَا تَكُونُواْ كَٱلَّذِينَ خَرَجُواْ مِن دِيَٰرِهِم بَطَرٗا وَرِئَآءَ ٱلنَّاسِ وَيَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِۚ وَٱللَّهُ بِمَا يَعۡمَلُونَ مُحِيطٞ
Wala msiwe kama wale walio toka majumbani mwao kwa fakhari na kujionyesha kwa watu, na wakawazuilia watu Njia ya Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ameyazunguka yote wanayo yafanya.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Msiwe kama mfano wa washirikina ambao walitoka nchini mwao kwa majivuno na kujionyesha ili wawazuie watu wasiingie kwenye dini ya Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu kwa wanayoyafanya ni Mwenye kuyazunguka. Hakifichiki Kwake chochote.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس