إِذۡ يَقُولُ ٱلۡمُنَٰفِقُونَ وَٱلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ غَرَّ هَـٰٓؤُلَآءِ دِينُهُمۡۗ وَمَن يَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِ فَإِنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٌ حَكِيمٞ
Na walipo sema wanaafiki, na wale wenye ugonjwa nyoyoni mwao: Watu hawa dini yao imewadanganya. Na Mwenye kumtegemea Mwenyezi Mungu basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Ametukuka, na Mwenye hikima.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kumbukeni waliposema watu wenye shaka na unafiki na wagonjwa wa nyoyo, huku wauona uchache wa Waislamu na wingi wa maadui wao, «Imewadanganya hawa Waislamu dini yao, ndipo ikawaingiza kwenye matatizo haya.» Na hawa wanafiki hawakuelewa kwamba mwenye kumtegemea Mwenyezi Mungu na akawa na uhakika wa ahadi Yake, basi Mwenyezi Mungu Hatamuacha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye ushindi, hakuna chochote kinachomshinda, ni Mwenye hekima katika uendeshaji Wake mambo na utengezaji Wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس