فَإِمَّا تَثۡقَفَنَّهُمۡ فِي ٱلۡحَرۡبِ فَشَرِّدۡ بِهِم مَّنۡ خَلۡفَهُمۡ لَعَلَّهُمۡ يَذَّكَّرُونَ
Basi ukiwakuta vitani wakimbize walio nyuma yao ili wapate kukumbuka.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Pindi utakapopambana na hawa, wanaovunja ahadi na mapatano, katika vita, wape adhabu ambayo itatia kicho kwenye nyoyo za wegine na itaitawanya mikusanyiko yao, huenda wao wakazingatia wasiwe na ujasiri wa kufanya kama yale waliyoyafanya waliotangulia.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس