يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّبِيُّ قُل لِّمَن فِيٓ أَيۡدِيكُم مِّنَ ٱلۡأَسۡرَىٰٓ إِن يَعۡلَمِ ٱللَّهُ فِي قُلُوبِكُمۡ خَيۡرٗا يُؤۡتِكُمۡ خَيۡرٗا مِّمَّآ أُخِذَ مِنكُمۡ وَيَغۡفِرۡ لَكُمۡۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Ewe Nabii! Waambie mateka waliomo mikononi mwenu: Kama Mwenyezi akiona kheri yoyote nyoyoni mwenu atakupeni bora kuliko vilivyo chukuliwa kwenu, na atakusameheni. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ewe Nabii, waambie mliowateka siku ya vita vya Badr, «Msisikitike juu ya fidia iliyochukuliwa kutoka kwenu. Iwapo Mwenyezi Mungu Aliyetukuka Atajua kwamba kwenye nyoyo zenu pana wema, basi Atawapa kilicho bora zaidi kuliko mali yaliyochukuliwa kutoka kwenu, kwa kuwarahisishia nyinyi, kwa hisani Yake, wema mwingi - Mwenyezi Mungu Alitekeleza ahadi Yake kwa 'Abbas, Mwenyezi Mungu Awe radhi naye, na wengineo- na Atawasamehe madhambi yenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa msamaha wa madhambi ya waja Wake wanapotubia, ni Mwenye huruma kwao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس