وَإِن يُرِيدُواْ خِيَانَتَكَ فَقَدۡ خَانُواْ ٱللَّهَ مِن قَبۡلُ فَأَمۡكَنَ مِنۡهُمۡۗ وَٱللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ
Ikiwa wanataka kukufanyia khiana, wao walikwisha mfanyia khiana Mwenyezi Mungu kabla yake, na Yeye akakuwezesha kuwashinda. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua Mwenye hikima.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wakitaka kukwendea kinyume mara nyingine, wale uliowaacha huru miongoni mwa mateka, basi usikate tamaa. Kwani wao tangu hapo walikuwa wamefanya uhaini kwa Mwenyezi Mungu na wakakupiga vita., na Mwenyezi Mungu Akakupa ushindi juu yao. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani, ni Mwenye hekima katika kuendesha mambo ya waja Wake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس