مَّلۡعُونِينَۖ أَيۡنَمَا ثُقِفُوٓاْ أُخِذُواْ وَقُتِّلُواْ تَقۡتِيلٗا
Wamelaanika! Popote watakapo onekana watakamatwa na watauliwa kabisa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hali ya kuwa wamefukuzwa kwenye rehema ya Mwenyezi Mungu; mahali popote watakapopatikana watekwe na wawe ni wenye kuuawa muda wa kuendelea kwao katika unafiki na kueneza habari za urongo baina ya Waislamu kwa lengo la kuleta fitina na uharibifu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس