وَٱلَّذِينَ سَعَوۡ فِيٓ ءَايَٰتِنَا مُعَٰجِزِينَ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمۡ عَذَابٞ مِّن رِّجۡزٍ أَلِيمٞ
Na wale walio jitahidi kuzipinga Ishara zetu wakaona watashinda, hao watapata adhabu mbaya yenye uchungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wale wanaotembea katika kuizuia njia ya Mwenyezi Mungu, kuwakanusha Mitume Wake na kuzitangua aya zetu huku wakiteta na Mwenyezi Mungu wakipinga amri Zake, hao watakuwa na adhabu mbaya zaidi na yenye ukali mwingi zaidi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس