أَوَلَمۡ يَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ يَبۡسُطُ ٱلرِّزۡقَ لِمَن يَشَآءُ وَيَقۡدِرُۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ
Kwani wao hawajui kwamba Mwenyezi Mungu humkunjulia riziki amtakaye na akamkadiria? Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanao amini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kwani hao hawajui kwamba riziki ya Mwenyezi Mungu kwa binadamu haimaanishi kuwa aliyeruzukiwa ana hali njema na kwamba Mwenyezi Mungu Ana hekima nyingi, Anamkunjulia riziki Anayemtaka katika waja Wake, awe mwema au muovu, na Anambania Anayemtaka katika wao? Hakika katika kukunjua na kubana riziki kuna dalili zilizo wazi kwa watu wanaoamini amri ya Mwenyezi Mungu na kuifanyia kazi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس