أَن تَقُولَ نَفۡسٞ يَٰحَسۡرَتَىٰ عَلَىٰ مَا فَرَّطتُ فِي جَنۢبِ ٱللَّهِ وَإِن كُنتُ لَمِنَ ٱلسَّـٰخِرِينَ
Isije ikasema nafsi: Ee majuto yangu kwa yale niliyo poteza upande wa Mwenyezi Mungu, na hakika nilikuwa miongoni mwa wanao fanya maskhara!
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Na mtiini Mola wenu na tubieni Kwake ili isije nafsi ikajuta na ikasema, ‘Ee hasara yangu kwa matendo mema niliyoyapoteza ulimwenguni katika yale Aliyoamrisha Mwenyezi Mungu na nikafanya kasoro katika kumtii na kutekeleza haki Yake,! Na ingawa ulimwenguni nilikuwa ni miongoni mwa waliokuwa wakiifanyia shere amri ya Mwenyezi Mungu, Kitabu Chake, Mtume Wake na waliomuamini.’
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس