قَدۡ سَأَلَهَا قَوۡمٞ مِّن قَبۡلِكُمۡ ثُمَّ أَصۡبَحُواْ بِهَا كَٰفِرِينَ
Waliyauliza hayo watu wa kabla yenu, kisha wakawa wenye kuyakataa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mfano wa maswali hayo, waliwahi waliokuwa kabla yenu kuwauliza Mitume wao. Walipoamrishwa yale waliokuwa wakiyauliza waliyakanusha na wasiyatekeleze. Basi, tahadharini msiwe kama wao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس