إِذۡ قَالَ ٱلۡحَوَارِيُّونَ يَٰعِيسَى ٱبۡنَ مَرۡيَمَ هَلۡ يَسۡتَطِيعُ رَبُّكَ أَن يُنَزِّلَ عَلَيۡنَا مَآئِدَةٗ مِّنَ ٱلسَّمَآءِۖ قَالَ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ
Wanafunzi walipo sema: Ewe Isa bin Maryamu! Je, Mola wako Mlezi anaweza kututeremshia chakula kutoka mbinguni? Akasema: Mcheni Mwenyezi Mungu ikiwa nyinyi ni Waumini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na ukumbuke waliposema Ḥawāriyyūn (wasafiwa wa Nabii ‘Īsā kati ya wafuasi wake), «Ewe ‘Īsā mwana wa Maryam! Je, Anaweza Mola wako, ukimuomba, kututeremshia meza ya chakula kutoka mbinguni?» Jawabu yake ilikuwa ni kuwataka wao wajikinge na adhabu ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, wakiwa ni wenye kuamini Imani ya kikweli.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس