قُلۡ أَتَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ مَا لَا يَمۡلِكُ لَكُمۡ ضَرّٗا وَلَا نَفۡعٗاۚ وَٱللَّهُ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ
Sema: Je! Mnawaabudu, badala ya Mwenyezi Mungu, wale ambao hawawezi kukudhuruni wala kukufaeni? Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kujua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sema, ewe Mtume, kuwaambia makafiri hawa, «Vipi mtamshirikisha Mwenyezi Mungu na asiyeweza kuwadhuru chochote wala kuwaletea manufaa yoyote?» Mwenyezi Mungu Ndiye Mwenye kuyasikia maneno ya waja Wake, Ndiye Mwenye kuzijua hali zao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس