وَمَن يُوَلِّهِمۡ يَوۡمَئِذٖ دُبُرَهُۥٓ إِلَّا مُتَحَرِّفٗا لِّقِتَالٍ أَوۡ مُتَحَيِّزًا إِلَىٰ فِئَةٖ فَقَدۡ بَآءَ بِغَضَبٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَمَأۡوَىٰهُ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ
Na atakaye wageuzia mgongo wake siku hiyo - isipo kuwa kwa mbinu za vita au kuungana na kikosi - basi atakuwa amestahiki ghadhabu ya Mwenyezi Mungu. Na pahala pake ni Jahannamu, na huo ni mwisho muovu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na yoyote katika nyinyi atawapa mgongo wake kwenye vita, isipokuwa kwa kupenya kama mbinu ya vita ya kuwachimba makafiri au kujiunga na mjumuiko wa Waislamu waliyo vitani popote waliopo, basi huyo amestahili kukasirikiwa na Mwenyezi Mungu, na makao yake ni Moto wa Jahanamu ambao ni mahali pabaya sana pa kuishia na kukomea.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس