۞إِنَّ شَرَّ ٱلدَّوَآبِّ عِندَ ٱللَّهِ ٱلصُّمُّ ٱلۡبُكۡمُ ٱلَّذِينَ لَا يَعۡقِلُونَ
Hakika vinyama viovu mbele ya Mwenyezi Mungu ni vile viziwi na bubu visio tumia akili zao.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika waovu zaidi wa wanaotembea kwenye ardhi, miongoni mwa viumbe vya Mwenyezi Mungu, mbele ya Mwenyezi Mungu ni viziwi ambao masikio yao yamezibana kutoisikia haki wakawa hawasikii, mabubu ambao ndimi zao zimeshikwa kutoitamka haki wakawa hawatamki. Hawa ndio wale wasioelewa maamrisho na makatazo yanayotoka kwa Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس