وَلَوۡ عَلِمَ ٱللَّهُ فِيهِمۡ خَيۡرٗا لَّأَسۡمَعَهُمۡۖ وَلَوۡ أَسۡمَعَهُمۡ لَتَوَلَّواْ وَّهُم مُّعۡرِضُونَ
Na Mwenyezi Mungu angeli jua wema wowote kwao ange wasikilizisha, na lau ange wasikilizisha wangeli geuka wakapuuza.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na lau Mwenyezi Mungu Alijua kwamba ndani ya hawa kuna kheri yoyote Angaliwafanya wasikie mawaidha ya Qur’ani na mazingatio yake mpaka wazifahamu hoja na dalili za Mwenyezi Mungu, Aliyeshinda na kutukuka. Lakini Yeye Alijua kwamba hamna kheri kwao na kwamba wao hawataamini. Na lau Aliwasikilizisha, kwa kukadiria na kukisia, wangaliipa mgongo Imani kwa kusudi na ujeuri, baada kuielewa. Na wao ni wenye kuipa mgongo, hawazunguki kuitazama haki kwa njia yoyote.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس